Pages

Saturday, July 14, 2012

NI VITA...




MCHEZO ULIVYOANZA
Akizungumza na…



MCHEZO ULIVYOANZA
Akizungumza na mapaparazi wetu juzikati, jijini Dar, Mchungaji Mwamkamba alisema awali alitoa matangazo na pia kutuma ujumbe mfupi wa simu ‘SMS’ kwa watu mbalimbali akiomba mchango wa fedha ili aweze kujenga kanisa lake, lakini bila matarajio yake, namba zake ziliangukia mikononi mwa watu hao.
“Nilitarajia kupanua kanisa langu hivyo nilihitaji mchango wa fedha kwa ajili ya ujenzi, nikatoa tangazo kwa watu mbalimbali pamoja na kutuma SMS kwa marafiki zangu.
“Siku moja nilipigiwa simu na watu nisiowajua, wakaniambia wanataka kukutana na mimi ili wanisaidie fedha  za ujenzi wa kanisa langu.
“Nilikubali, nikaenda kukutana nao pale Ubungo. Walianza kunieleza jinsi walivyoamua kunisaidia kujenga hekalu la Mungu huku wakisema wananipa fedha za kutosha na kuagana na umaskini,” alisema Mchungaji Mwamkamba.
Aliendelea kudai kuwa watu hao walisema lengo lao ni kumpa kiasi chochote cha fedha ambacho kilikuwemo kwenye ‘brifkesi’ kwa ajili ya ujenzi huo.
“Waniliambia wananipa kiasi chochote cha fedha ninachokihitaji, lakini iwe siri yangu na wao, halafu wakasema waumini katika kanisa langu wataongezeka.

MCHUNGAJI AZIDI KUFICHUA
“Wakaniambia wamefanya hivyo kwa watumishi wengi wa Mungu hapa Tanzania ambao kwa macho ya kawaida huwatambuliki kama ni wafuasi wa Freemason na wanafanya ishara na miujiza mingi huku makanisa yao yakiwa na idadi kubwa ya waumini.”
APEWA MKATABA
Baada ya mazungumzo ya muda mrefu na kabla mchungaji huyo hajasema ndiyo au hapana, alipewa mkataba wenye maelekezo ya jinsi ya kujiunga ili aanze kula mema ya nchi na kuuaga umaskini kwa muda mfupi.
“Walinipa mkataba, una nembo ya Freemason, lakini wakaniambia ni lazima nibadili dini, nianze kuvaa nembo ya mwewe na nyoka na kumtoa kafara mke wangu au mwanangu nimpendaye kama sadaka ya shukrani kwa mungu wao,” alisema mchungaji.
AWACHOMOLEA WAZI
“Niliposikia masharti hayo, ghafla nilisikia uchungu moyoni, nikakataa, nilisimama haraka sana na kuondoka kwa mwendo wa haraka, kama nakimbia. Wakaanza kunizomea huku wakitoa ishara ya kuvunja vidole viwili ambayo ni moja ya alama za Freemason,” alisema mchungaji huyo.
KWA NINI NI VITA?
Hivi karibuni, Mchungaji wa Kanisa la Good News for All Nations, Mark Diganyeka alitoa alama za kuwatambua watumishi wa Mungu ambao ni waumini wa dini ya Freemason na kusema kuwa waumini wawe makini kuwabaini.
Miongoni mwa alama hizo alisema ni pamoja na kuvunja vidole kwa haraka wakati wakihubiri na kuvaa pete kubwa kwa ajili ya kufanyia miujiza wawapo madhabahuni.
Kwa tafsiri ya Mchungaji Diganyeka na hayo aliyokutana nayo Mchungaji Mwamkamba, ni dhahiri  makanisa yameingiliwa na Freemason hivyo kuanza kutimia kwa yale maneno kwamba, imani hiyo itawavaa watumishi wa Mungu kabla ya kurudi kwa Yesu Kristo.

AIBU TUPU...



Ni aibu tupu! Mnyange aliyeibuka mshindi wa pili kwenye kipute cha Miss Vyuo Vikuu au Miss Higher Learning 2012/13, Fatma Ramadhan (pichani), ameacha gumzo baada ya kukwea jukwaani akiwa kaacha wazi mlango wake wa ‘ikulu’ bila kufuli, Risasi Jumamosi linairusha hewani.
NI MBELE YA MBUNGE

Tukio hilo la aina yake lililoshuhudiwa na mwandishi wetu, lilijiri usiku wa kuamkia Julai 7, mwaka huu kwenye Ukumbi wa New Maisha uliopo Masaki, Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mbunge wa Kisesa kwa leseni ya CCM, Mhe. Luhaga Joelson Mpina.
Katika…


Ni aibu tupu! Mnyange aliyeibuka mshindi wa pili kwenye kipute cha Miss Vyuo Vikuu au Miss Higher Learning 2012/13, Fatma Ramadhan (pichani), ameacha gumzo baada ya kukwea jukwaani akiwa kaacha wazi mlango wake wa ‘ikulu’ bila kufuli, Risasi Jumamosi linairusha hewani.
NI MBELE YA MBUNGE
Tukio hilo la aina yake lililoshuhudiwa na mwandishi wetu, lilijiri usiku wa kuamkia Julai 7, mwaka huu kwenye Ukumbi wa New Maisha uliopo Masaki, Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mbunge wa Kisesa kwa leseni ya CCM, Mhe. Luhaga Joelson Mpina.
Katika tukio hilo ambalo hata mheshimiwa mbunge aliliona na kutazama pembeni, ilifahamika kuwa mrembo huyo aliyetimba jukwaani akiwa hajavaa nguo ya ndani, alitokea kwenye Chuo Cha Uandishi wa Habari mkoani Arusha.
“Jamani… jamani! Yaani huyu binti yuko uchi kabisa, imekuwaje au kajisahau? Ni aibu iliyoje, tena mbele ya mheshimiwa mbunge? Hii kweli aibu tupu,” alisikika mmoja wa watazamaji wa kinyang’anyiro hicho.
RASHIDA NAYE AANIKA MAMBO
Katika tukio lingine la aibu kwenye ‘iventi’ hiyo, kivazi cha mkufunzi wa warembo ambaye ni Miss Mara 2000, Rashida Wanjara kiliacha watu midomo wazi baada ya kuanika mambo yake nyeti ya mwilini.
“Duh! Huyu naye kiboko. Yaani kila kitu mpaka vya chumbani kaviacha hadharani?”
HEBU MSIKIE
Risasi Jumamosi lilipomvaa na kumuuliza kulikoni kuvaa kigauni kinachoonesha maungo yake nyeti, alifunguka: “Mimi ndiye miss nisiyechuja, nikiamua kushiriki umiss bado nakubalika na mwili wangu unalipa.”

AFANDE SELE AKIFUNGUKA KUHUSU SHOW YA ZANZIBAR MUSIC AWARD

Salaam Ndugu zangu wote mashabiki na wadau wa muziki wetu!!
Tamko langu kuhusiana na lugha zilizotolewa na Twent Percent kuhusiana na show yetu ya Zanzibar Music Award.
"Tulialikwa kwenye ZANZIBAR MUSIC AWARD, na kabla ya kazi makubaliano yote ya kazi kwa mujibu wa mkataba yalifuatwa, makubaliano hayo yalihusisha sisi kujigharamia gharama zote za nauli na Malazi (accomodation).
Tulifika Zanzibar salama, tulipokua Zanzibar twenty alitaka agharamiwe huduma zote ambazo ni nje ya mkataba wetu, nikamuomba na kumsihi sana Ndugu yangu aheshimu mkataba, asitafute matatizo kwani tayari mpaka wakati huu tuna kesi na Halmashauri ya Manispaa ya Moro ambayo kimsingi sikuhusika (nilishatolea ufafanuzi siku za nyuma).
Lakini yeye alipingana na mimi, akanibishia na kunisukuma Mbele ya wageni na wenyeji wetu, wakiwemo Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seiph Ali Idi, Waziri Seiph Khatibu.
Walikuwepo waadishi wa habari wa siku Nyingi Akiwemo Abubakari Liongo (idhaa ya kiswahili radio Ujerumani), Mkurugenzi wa ZENJI FM ndugu Tua Saidi Tua.
Mimi Selemani Abdallah Juma Msindi sihusiki kwa namna yoyote, na tabia zisizo za kuridhisha zinazoonyeshwa na Ndugu yangu Twenty Percent, ambae nimekua nae nyumbani kwangu hata kabla ya Tuzo zake Tano (Kili Music Award) ambazo kazi hizo zote hizo kaandikia nyumbani kwangu siwezi kuwa na tatizo nae ni ndugu yangu kiimani na kikazi, hata kazi yangu niliyofanya nae kabla siku za nyuma "MBELE YAKO NYUMA YANGU" .. Kuna mstari Nilisema " ..Kuandika Rhyme kwenda Gym kimtindo kuonyesha Ugum, bado unatakiwa uwe na nidhamu ya kweli, sio ya kumzuga Mwalimu, utajihukumu".
Nimekua nikisisitiza nidhamu kwa Ndugu zangu woote toka enzi za Ghetto BoyZ, Watupori na Mabwasha'Kingdom, ambao wengine hawafanyi sanaa, ila nipo nao kwenye Familia yetu kubwa hapa Tanzania. Nimesikitishwa na kitendo hicho. Siku zote nimekua mwenye kuhitaji suluhu kwa namna ya Amani.
Verry sorry kwa wote ambao mumefadhaika kwa hilo. Tuendelee kuwa pamoja na msisite kutoa ushauri wenu, maoni ili Game letu lisonge. MUNGU ATUBARIKI.
Asanteni sana.
Selemani Juma Abdallah Mutabhazi Msindi.
a.k.a Afande Sele (King of Rhymes)
 

Blogger news

Search This Blog

Blogroll

Follow by Email

About